Habari
-
17.05.2022Maonesho ya Elimu ya Umoja wa Ulaya jijini Dar es SalaamUbalozi wa Poland ulishiriki kikamilifu katika Maonesho ya Elimu ya Umoja wa Ulaya ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Ulaya nchini Tanzania yaliyoandaliwa na wawakilishi wa Umoja wa Ulaya.
-
15.05.2022Maadhimisho ya Siku ya Ulaya nchini TanzaniaMnano tarehe 9 Mei, 2022, tuliadhimisha Siku ya Ulaya jijini Dar es Salaam. Katika tafrija hiyo iliyohudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje, LiberataMulamula, Mabalozi wa Umoja wa Ulaya na wageni mbalimbali, maonesho ya picha za miradi ya maendeleo inayotekelezwa nchini Tanzania na Nchi Wanachama yaliwasilishwa.
-
07.05.2022Maadhimisho ya miaka 231 tangu kupitishwa kwa Katiba ya Tarehe 3 Mei na siku ya Wapoland waishio nchini TanzaniaWakati wa tafrija iliyoandaliwa katika bustani za Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam, Balozi Krzysztof Buzalski alirejelea historia ya kupitishwa kwa Katiba ya tarehe 3 Me na kusoma barua kutoka kwa Waziri SzynkowskivelSęk yenye pia ujumbe wa kuwatakia kila la kheri wakazi wote wenye asili ya Kipoland waishio nchini.
-
06.04.2022Msaada wa Kipoland unasaidia kuboresha elimu, usafi na mazingira ya usafi wa jamii katika eneo la KiabakariUpande wa Kaskazini – Magharibi mwa Tanzania – huko Kiabakari – miradi miwili ya maendeleo iliyofadhiliwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Poland katika mashindano ya Polish Development Aid ya 2021 na kutekelezwa na Kiabakari Foundation pamoja na Parokia ya Kikatoliki ya Kiabakari imezinduliwa.
-
25.03.2022Tamasha la Wasanii wa Poland na Tanzania wakati wa Toleo la Pili la Tamasha la Pamoja ZanzibarMnamo Machi 23, 2022, katika ukumbi wa Alliance Francaise jijini Dar es Salaam, tulifurahi kusikiliza tamasha la wasanii wa Poland na Tanzania ikiwa ni sehemu ya tamasha la 2 la Pamoja Zanzibar, lililoandaliwa na Radek Bond Bednarz na kuungwa mkono na Ubalozi wetu. Balozi Buzalski alijitolea tamasha kwa ajiri ya wahasiriwa wa vita huko Ukraine.
-
21.01.2022Tunafanya kazi kuongeza ujasiriamali wa wakazi wa Usandawe na kulinda sanaa ya miamba katika Hifadhi ya Swaga SwagaShukrani kwa ushiriki wa mwanaakiolojia wa Poland Maciej Grzelczyk na ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa mwaka 2021 mradi uliotekelezwa kama sehemu ya misaada ya Kipolandi yenye lengo la kuamsha na kuelimisha wakazi wa eneo la Usandawe nchini Tanzania kwa ajili ya kulinda sanaa ya miamba na urithi wa kitamaduni wa jamii ya Wasandawe umekamilika.
-
28.12.2021Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam utafungwa Januari 6-7, 2022Tunapenda kuwafahamisha kuwa ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam utafungwa tarehe 6-7 Januari 2022.
-
28.12.2021Makaburi mengine ya Poland nchini Tanzania - huko Kidugala - yamekarabatiwaShukrania kwa ushirikiano wa Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam, kituo cha nyaraka,ufukuzwaji na uhamisho wa Chuo Kikuu cha Pedagogical huko Cracow,wakfu wa PU “pro Univesitatis” na Wizara ya Utamaduni na Urithi wa kitaifa, makaburi mengine ya Poland nchini Tanzania yamekaratiwa.
-
09.12.2021Shukrani kwa Mfuko wa Msaada wa Poland, Watoto kutoka katika Milima ya Usambara tayari wanafaidika na chumba cha pili cha ziada cha mtaala wa kawaidaMwaka huu, Shukrani kwa ushiriki wa mshirika wa ndani -A.D. Views Management Ltd. na fedha zilizochangwa kama sehemu ya ushirikiano wa maendeleo wa Poland na Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es salaam, tayari takribani wasichana na wavulana 300 kutoka wilaya ya Lushoto katika milima ya Usambara kaskazini mwa Tanzania wanahudhuria vyumba vilivyopangwa maalum vinavyotoa sio tu mahali salama pa kucheza, lakini juu ya yote kujifunza.
-
05.12.2021Mfuko wa misaada wa Poland kuendelea kuisaidia Tanzania katika mapambano yake dhidi ya Kifua KikuuUlinzi wa afya ni mojawapo ya vipaumbele vya ushirikiano wa maendeleo wa Poland na nchi za Afrika. Ndio maana mwaka huu tunaendelea kufadhili mradi wa shirika la APOPO unaotekelezwa nchini Tanzania, unaojumuisha kugundua ugonjwa wa kifua kikuu kwa msaada wa panya wakubwa wa kusini.