Ili kuhakikisha huduma bora zaidi, tunatumia faili ndogo zinazoitwa kuki. Wakati wa kutumia wavuti yetu, faili za kuki zinapakuliwa kwenye kifaa chako. Unaweza kubadilisha mipangilio ya kivinjari chako wakati wowote. Kwa kuongezea, utumiaji wako wa wavuti yetu ni sawa na idhini yako kwa usindikaji wa data yako ya kibinafsi inayotolewa na njia za elektroniki.
Kwenda Nyuma

Kompyuta mpakato mpya za Shule ya Awali na Msingi ya St. Gertrude iliyopo Kilimahewa

01.09.2025

Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam unasaidia maendeleo ya elimu ya kidijitali nchini Tanzania kupitia miradi inayofadhiliwa na Polish Aid.

Children working on new laptops in St. Getrude Pre & Primary school

Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam unaendelea na juhudi za kuimarisha elimu nchini Tanzania.

Ijumaa iliyopita, mwakilishi wa Ubalozi, Katarzyna Sobiecka, alitembelea Shule ya Awali na Msingi ya St. Gertrude iliyopo Kilimahewa (PWANI) ambayo inashukuru kwa msaada wa Ubalozi wetu na Shirika la Polish Aid wa kompyuta mpakato mpya 14. Kompyuta zilizotolewa zitasaidia wanafunzi kupata ujuzi wa kidijitali kwa vitendo, wakati walimu wataweza kukuza zaidi ujuzi wao wa kitaaluma.

Mradi huu unachangia maendeleo ya rasilimali watu na unasaidia ujenzi wa jamii ya kisasa ya kidijitali nchini Tanzania, kulingana na vipaumbele vya serikali ya Tanzania.

Picha (7)

{"register":{"columns":[]}}