Habari
-
09.01.2026Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam umefungwa tarehe 12 Januari 2026Kitengo cha Viza cha Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam kitakuwa imefungwa tarehe 12 Januari 2026 kutokana na sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar.
-
05.01.2026Kuimarisha Huduma ya Dharura nchini Tanzania kupitia Msaada wa Polish AidChini ya mradi uliyodhaminiwa na Polish aid, vifaa vya matibabu viliwasilishwa katika hospitali mbili za mkoa wa Dar es Salaam na vile vile kwa Kituo cha Mafunzo ya Madawa ya Dharura ya Tanzania-Poland na kuimarisha mfumo wa huduma ya dharura ya matibabu ya Tanzania.
-
10.12.2025 OltotoiMsaada wa Polish aid Kuendeleza Huduma za Afya OltotoiMradi wa mwaka huu, unaofadhiliwa na Msaada wa Poland katika wilaya ya Ndotoi, Tanzania, ulikuwa na lengo kuu la kuongeza fursa za wanawake wa hapa kupata uchunguzi sahihi na kinga dhidi ya magonjwa ya kuambukiza.
-
08.12.2025Maonesho ya "JUICE Tanzania" ya Mickey WyrozebskiTarehe 6 Desemba, maonesho ya "JUICE Tanzania" yaliyoandaliwa na mtaalamu wa upigaji picha kutoka Poland, Mickey Wyrozębski yalifunguliwa rasmi katika Nafasi Art Space, Dar es Salaam. Ufunguzi hiyo ilifanyika chini ya Udhamini wa Heshima wa Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam.
-
04.12.2025 SegereaMsaada wa Polish Aid umewezesha vijana wa Segerea kutumia maktaba mpyaMnamo mwaka 2025, kwa ufadhili wa Polish Aid, ilizinduliwa maktaba mpya katika Kituo cha Elimu cha St. Maximilian huko Segerea na kupatiwa vifaa, na hivyo kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi wa kidato cha sekondari.
-
03.12.2025Mfuko wa Polish Aid kusaidia kilimo chenye ufanisi zaidi katika Mkoa wa KilimanjaroMwaka huu, Polish Aid ilisaidia mradi unaolenga kuzindua mfumo wa kisasa wa umwagiliaji kwa mashamba ya mahindi ya Kituo cha Mafunzo ya Kilimo na Mifugo cha Kilacha (KALTC).
-
01.12.2025Jumuiya ya Wapoland nchini Tanzania iliadhimisha miaka 107 ya Uhuru wa PolandTarehe 28 Novemba, Ubalozi uliandaa tafrija maalum ya kuadhimisha miaka 107 ya Poland kupata uhuru na kuwakusanyisha wanajumuiya ya kipoland nchini Tanzania, pamoja na wahitimu wa kitanzania wa vyuo vikuu vya Polandi.
-
24.11.2025 Dar es SalaamOnyesho la Filamu ya 'Miungu' wakati wa kumbukumbu ya miaka 40 ya upandikizaji wa moyo wa kwanza kufanikiwa PolandiTarehe 17 Novemba 2025 tuliandaa onyesho la filamu ya Kipoland "Gods," ('Miungu') tukiadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 ya mafanikio makubwa ya Prof. Zbigniew Religa - upandikizaji wa moyo wa kwanza kufanikiwa nchini Polandi.
-
24.11.2025Polish Aid inasaidia ujasiriamali na elimu ya mazingira katika Bonde la KilomberoTulitembelea bonde la Kilombero, Tanzania, kufuatilia mradi unaotekelezwa kwa ushirikiano na Mradi wa Tembo Kusini mwa Tanzania (STEP), wenye lengo la kuimarisha ujasiriamali na kukuza elimu ya mazingira mkoani humo.
-
07.11.2025Ubalozi wa Jamhuri ya Poland mjini Dar es Salaam utakuwa umefungwa tarehe 10 na 11 Novemba 2025Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam, pamoja na Kitengo cha Viza, zitakuwa zimefungwa tarehe 10 na 11 Novemba 2025 kutokana na sikukuu za kitaifa.