Habari
-
29.11.2024Konseli wa Jamhuri ya Poland Wojciech Łysak alitembelea maeneo yenye miradi ya maendeleo yanayoungwa mkono na Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam kwa ufadhili wa mfuko wa Polish Aid katika msitu wa Magombera
-
01.11.2024Kuadhimisha Sikukuu ya Watakatifu Wote, kaimu balozi Katarzyna Sobiecka na mkuu wa idara ya utawala na uhasibu, Bw. Edgar Klusa waliweka maua kwenye makaburi ya ndugu Makaburini Kinondoni, Dar es Salaam. Konseli wa Jamhuri ya Poland, Wojciech Łysak alitembelea makaburi ya wapolish yaliyopo Ifunda, karibu na Iringa, na Konseli msaidizi Krystyna Fatyga alitembelea makaburi ya Wapoland yaliyopo Bigwa, karibu na Morogoro.
-
22.08.2024Matatizo ya kiafya, ukosefu wa elimu stahiki na ujuzi wa kitaalamu unaowakwamisha kupata ajira, pamoja na kutengwa na jamii, bado ni changamoto kubwa zinazowakabili watu wenye ualbino nchini Tanzania. Mradi wa ‘Mustakabali bora kwa watu wenye ualbino nchini Tanzania’ unaofadhiliwa na Polish Aid kimsingi unalenga kuwapa watu hao nafasi sawa za kuishi maisha bora.
-
07.08.2024Ufunguzi wa Kongamano la Kiesperanto la Dunia nchini Tanzania kwa Ushiriki wa Mwakilishi wa Ubalozi.Kongamano la Dunia la Kiesperanto lililofanyika jijini Arusha kuanzia Agosti 3-10 mwaka huu, limewakutanisha zaidi ya wazungumzaji mia saba sabini wa lugha ya Esperanto kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Ufunguzi wa tukio hili la kipekee, lenye lengo la kukuza uelewa wa kimataifa na kubadilishana utamaduni, pia ulihudhuriwa na mwakilishi wa ubalozi wetu - Naibu Konseli Krystyna Fatyga.
-
06.08.2024Naibu Konseli wa Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam, Krystyna Fatyga, alipotembelea makaburi ya wakimbizi wa Poland yaliyopo Tengeru pamoja na washiriki wa Kongamano la Dunia la Kiesperanto, lililofanyika mwaka huu jijini Arusha.
-
28.06.2024Ubalozi wa Poland jijini Dar es Salaam uliandaa uangaliaji wa pamoja za mechi za Poland katika hatua ya makundi wakati wa Mashindano ya mpira wa migu ya Ulaya.
-
03.05.2024Wakati wa tafrija iliyoandaliwa katika bustani ya Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam, Balozi Krzysztof Buzalski alirejelea historia ya kupitishwa kwa Katiba ya tarehe 3 Mei na kufafanua zaidi kuhusu historia ya Poland pamoja na mafanikio ya kijamii na kiuchumi ya nchi hiyo baada ya kujiunga na Umoja wa Ulaya mnamo Mei 1, 2004. Pia, alisisitiza uimara wa mungano na Ukraine inayojihami dhidi ya mashambulizi ya Urusi huku ikipigania kujiunga na ulimwengu wa kidemokrasia.
-
01.03.2024Kama sehemu ya ushirikiano na EUNIC (Taasisi za Kitaifa za Utamaduni za Umoja wa Ulaya) nchini Tanzania, tulishiriki katika utekelezaji wa mradi wa "Viraka Freshi/Vipande Vipya", unaounga mkono vijana wabunifu wa Kitanzania katika sekta ya uzalishaji wa chapa mbalimbali na endelevu za kimitindo. Washirika waliounga mkono mradi ni mabalozi ya: Ufaransa, Hispania, Ujerumani, Italia, Ireland, Poland na Umoja wa Ulaya - EU, pamoja na mashirika ya Alliance Francaise, Goethe Institut na British Council, na pia mashirika ya ndani ya nchi kama vile Naledi Creative Center na CDEA Fashion Incubator.
-
09.02.2024Mnamo Februari 8-9, 2024, Rais Andrzej Duda na Mke wa Rais Agata Kornhauser-Duda walifanya ziara rasmi nchini Tanzania, ambapo yalifanyika mazungumzo na Rais Samia Suluhu Hassan, kutembelea Hospitali ya Aga Khan inapotekelezwa mradi kupitia Misaada ya Poland, pamoja na kushiriki katika tafrija ya wanajamii wa Poland.