Habari
-
25.11.2021Tamasha la piano kwenye hafla ya Mwaka wa ChopinKama sehemu ya kusherehekea Mwaka wa Chopin, tarehe 24 mwezi wa 11 mwaka 2021, Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es salaam uliandaa tamasha la piano kwa ushirikiano na Ubalozi wa Ujerumani lililochezwa na mpiga kinanda mahiri wa Poland Jan Krzysztof Broja.
-
12.11.2021Tuliadhimisha Siku ya Uhuru waTanzaniaWakati wa tafrija ya sherehe za kuadhimisha miaka 103 ya kupata uhuru iliyoandaliwa katika bustani za ubalozi wa Jamhuri Poland jijini Dar es salaam, Balozi Krzysztof Buzalski alisoma barua kutoka kwa Waziri SzymonSzynkowskivelSęk yenye kuwatakia kheri wanadiaspora wa Poland duniani na alikumbuka historia ya kurejesha uhuru.
-
01.11.2021Ziara ya Siku ya Watakatifu Wote katika makaburi ya Tengeru na KinondoniSiku ya Watakatifu wote ilikua ni hafla ya kuwakumbuka watu waliohamishwa kutoka Poland kutokana na Vita vya Pili vya Dunia nchini Tanzania. Balozi Krzystof Buzalski pamoja na wajumbe kutoka Wizara ya Utamaduni na Urithi wa Taifa waliweka shada la maua katika makaburi ya Tengeru, na wawakilishi wengine wa ubalozi walitembelea makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
-
29.10.2021Onyesho la filamu ya “Sweat” katika Tamasha la Filamu la UlayaIkiwa ni sehemu ya Tamasha la Filamu la Ulaya, lililoungana na Tamasha la Kimataifa la Filamu visiwani Zanzibar, Oktoba 29, 2021, Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es Salaam uliandaa onyesho la filamu iliyoshinda tuzo. “Sweat” katika Taasisi ya Ufaransa iliyopo nchini Tanzania.
-
22.10.2021Shukrani kwa msaada wa Wapoland, Tunaandaa jengo jipya la Chekechea- ‘Holy Family Day Care’ huko SegereaFenicha mpya za shule, magodoro pamoja na jiko, vifaa vya kufulia na uwanja wa michezo vitahudumia watoto wadogo kutoka Segerea hivi karibuni, Wilaya ya Dar es Salaam, pamoja na wafanyakazi wa shule wanaofanya kazi katika shule ya chekechea. Ununuzi wa vitu vya msaada wa Poland utawawezesha Masista Wamisionari wa Familia Takatifu kufungua hivi karibuni jengo jipya la Chekechea-Holy Family Day Care.
-
09.10.2021Msaada wa Poland kusaidia uwezeshwaji wa muingiliano wa maisha ya binadamu na tembo katika Bonde la Kilombero nchini TanzaniaKatika ratiba ya utendaji kazi wa msaada wa Kipoland, Ubalozi wa Jamuhuri ya Poland Dar es Salaam unawezesha hatua za shughuli za mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yanafanya kazi kwa manufaa ya kuboresha muingiliano wa kimaisha wa watu na tembo katika Bonde la Kilombero. Lengo ni kutafuta ufumbuzi katika eneo la mwingiliano wa kimaisha baina ya wanyama na jamii ya wenyeji, kwa kuzingatia tatizo linalosababishwa na upanuzi wa makazi ya watu na kilimo kwenye maeneo ambayo wanyama hao wapo, kwa mfano kando kando ya mipaka ya maeneo hifadhi.
-
23.09.2021Kituo cha huduma cha St. Angel Day Care na basi jipya la shule lililofadhiliwa na msaada wa PolandBasi jipya la kituo cha kulelea watoto cha St. Angel Day Care kilichopo Kurasini, Dar es Salaam, limenunuliwa katika mfumo wa mradi wenye kichwa kisemacho “kuongeza fursa za elimu kwa watoto kurasini kwa kusaidia vyombo vya usafirishaji” kwa wengine kutoka katika mfuko wa misaada wa Poland.
-
20.09.2021Tunajiunga na Siku ya Usafi Duniani nchini TanzaniaJumamosi Septemba 18, Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es salaam kwa mara nyingine ulijiunga na Siku ya Usafi Duniani nchini Tanzania.
-
08.09.2021Wanafunzi kumi na mbili wa Kitanzania kupatiwa udhamini chini ya programu ya BanachBalozi Krzysztof Buzalski na Konsul Piotr Kruze walikutana Septemba 8, 2021, kundi la wanafunzi wenye bahati kutoka Tanzania waliotunikiwa chini ya programu ya Banach, mpango wa pamoja wa Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Elimu na Sayansi na Wakala wa Taifa wa Poland wa ubadilishano wa Kitaaluma. Programu imeelekezwa kwa vijana kutoka katika nchi zinazoendelea ambao wangependa kuchukua masomo ya shahada ya udhamili nchini Poland.
-
16.07.2021Ubalozi ukiwasaidia wasanii wa Poland wakati wa Tamasha la Pamoja ZanzibarKatika nusu ya kwanza ya Julai 2021, tulipata furaha kuwakaribisha kundi la wasanii wa Poland waliotumbuiza wakati wa mfululizo wa matamasha kama sehemu ya Tamasha la Pamoja Zanzibar, lililoandaliwa na Radek Bond Bednarz, msanii na mtayarishaji wa Poland, mwanzilishi wa Eklektik jukwaa la kitamaduni, linalojulikana kwa shughuli zake huko Wraclaw.